Tarehe 29/9 ya kila mwaka ni siku ya maazimisho ya siku ya moyo duniani, siku ya moyo ni siku ambayo inazungumziwa afya ya moyo pamoja na mogonjwa mbali mbali ya moyo. Fahamu kwa ufupi baadhi ya magonjwa ya moyo na jinsi ya kujikinga na magonjwa hayo:
i. Magonjwa yanayoathiri mishipa ya damu ya moyo
ii. Magonjwa yanayoathiri misuli ya moyo
iii. Magonjwa ya valve za moyo
iiii. Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa
MAMBO AU VIHATARISHI VINAVYOONGEZA UWEZEKANO WA MTU KUPATA UGONJWA WA MOYO
i. Ugonjwa wa shinikizo kubwa la damu (Presha) hasa kama hautumii dawa na matibabu ya kudhibiti presha
ii. Ugonjwa wa kisukari
iii. MATUMIZI YA SIGARA: Hii ujumuisha uvutaji wa sigara,tumbaku na ugoro
iiii. LISHE MBAYA: Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi,sukari nyingi,chumvi nyingi, lehemu nyingi na kutotumia mbogamboga na matunda.
v. Unywaji pombe
vi. Uzito au unene uliopitiliza
vii. Kutokufanya mazoezi
viii. Umri : Zaidi ya miaka 50
ix. Historia ya ugonjwa wa moyo kwenye familia
x. JINSI: Jinsia ya kuime hupata ugonjwa wa moyo mapema
DALILI ZA UGONJWA WA MOYO
i. Maumivu ya kifua hasa yanayotembea mpaka kwenye mabega, shingo au taya
ii. Moyo kwenda mbio (Moyo kudunda kwa nguvu isivyo kawaida )
iii. Uchovu uliopitiliza, mwili kuwa dhaifu na kuchoka haraka hata kwenye shughuri ndogo
iiii. Kukosa pumzi au kushindwa kupumua vizuri hasa unapolala chali
v. Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji
vi. Tumbo kujaa, kichefuchefu na kutapika
vii. Kushindwa kulala vizuri hasa kushtuka usingizini kuhisi kama unakabwa na kukosa pumzi
Hizi ni baadhi ya dalili na mara nyingi mtu huanza kupata dalili wakati ameshaishi na ugonjwa kwa muda mrefu. Ni muhimu sana kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara.
JE UNAWEZA VIPI KUEPUKA UGONJWA WA MOYO AU KUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUPATA MARADHI HAYA?
Wataalamu wa tiba tunakubaliana kuwa njia nzuri ya kupambana na magonjwa ya moyo ni kuzuia yasitokee. Ni muhimu watu kuchukua hatua kuhusu vihatarishi vya magonjwa ya moyo kama ifuatavyo
1.LISHE
Japo kwa mara ya kwanza lishe bora huonekana kama jambo gumu ila baada ya mwili mwili huzoea na kufurahia chakula kama kawaida
i. Punguza vyakula vyenye wanga na sukari nyingi
ii. Punguza vyakula vyenye mafuta mengi hasa yale yanayotokana na wanyama
iii. Punguza ulaji wa nyama nyekundu kama ng’ombe, mbuzi inashauriwa kiasi cha nyama tunachokula kisizidi nusu kilo kwa wiki
iiii. Ongeza matumizi ya nafaka zisizokobolewa kama ugali wa dona,ulezi na mtama
v. Ongeza. ulaji wa vyakula jamii ya kunde, mbogamgoga na matunda
2.MAZOEZI
Kiwango cha mazoezi kinachoshauriwa kufanya ni walau dakika 30 kila siku. Kukaa bila kufanya mazoezi wala shughuri yoyote huuweka mwili katika hatari ya kupata magonjwa ya moyo
3.DHIBITI MATUMIZI YA VILEVI (POMBE NA SIGARA)
Epuka matumizi ya vilevi kama sigara na pombe. Kama mtumiaji wa pombe unatakiwa upunguze kabisa mpaka kiwango kinachoruhusiwa kitabibu
4. DHIBITI TATIZO LA PRESHA NA SUKARI
Ni vyema kuzingatia ushauri uliopewa na daktari kuhusu presha au kisukari pia na kuzingatia matumizi ya dawa kama ilivyoshauriwa na daktari.
5. MIKAZO (STRESS) ZA MAISHA
Mkazo (STRESS) uliopitiliza huuweka moyo katika hatari ya kupata maradhi. Ni vyema kutafuta namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo na mkazo
6. Jenga tabia ya kupima afya yako mara kwa mara.
Chanzo: Dr.Norman Jonas